Mradi mpya wa PIATA kuwekeza US$280M kwenye Kilimo Afrika Mashariki

Nchi za afrika mashariki zikiwemo Tanzania, Kenya, Ethiopia na Rwanda zitafaidika na program ya uwekezaji wa kifedha kwenye kilimo, yenye lengo la kuongeza kipato na usalama wa chakula kwa familia zaidi ya milioni 30 katika nchi 11 barani afrika mpaka mwaka 2021. Program hiyo ya Partnership for Inclusive Agricultural Transformation in Africa (PIATA), inatazamia kutoa kiasi cha Dola za kimarekani Milioni 280(US$280 Million) katika kuleta mapinduzi ya kilimo barani afrika.
Partnership for Inclusive Agricultural Transformation in Africa 
Program hiyo imezinduliwa hivi karibuni kwenye mkutano wa Mapinduzi ya kijani barani afrika yaani Africa Green Revolution Forum(AGRF) iliyofanyika wiki iliyopita nchini Ivory Coast; ambapo washiriki 3 wakubwa ambao ni Rockefeller Foundation, USAID na Taasisi ya Bill & Melinda Gates Foundation ndio watakaowezesha program hiyo. Programu hiyo itagusa katika kutengeneza mifumo ya kutoa pembejeo, mnyororo wa thamani na sera.
Bill & Melinda Gates Foundation
Mkurugenzi mtendaji wa Rockerfeller Foundation, bwana Mamadou Biteye, amesema ushiriki huo utasaidia wadau hao kusaidia maendeleo ya afrika na uwezeshaji kwa wananchi kuwa mkubwa kupitia mapinduzi ya sekta ya kilimo barani humo. "Tunategemea kupeka teknologia ambazo zitasaidia sekta ya kilimo kwa miaka kadhaa ijayo, kukusanya mawazo yetu na uzoefu ambao utasaidia kuwafikia watu wengi zaidi”
Mkurugenzi mtendaji wa Rockerfeller Foundation, bwana Mamadou Biteye

Kuanzishwa kwa mradi huo kutasaidia malengo ya Azimio la Maputo la mwaka 2014 la kuhamasisha uwekezaji wa kifedha kwenye sekta ya kilimo barani afrika. Nae bwana Sean Jones, mwakilishi kutoka USAID amesema PIATA itasaidia kuja na njia mpya ya kufanya biashara na kuhakikisha usalama wa chakula na ukuaji wa uchumi wa nchi husika.

Raisi wa Alliance for a Green Revolution in Africa, Bi Agnes Kalibata

Nae Agnes Kalibata, Rais wa Alliance for a Green Revolution in Africa, amesema uhusiano huo wa washiriki utasaidia sana ukuaji wa nchi husika na kutengeneza ajira kupitia sekta ya kilimo, kusaidia serikali kuwezesha wakulima wadogo wadogo na ukuaji wa kilimo biashara. Ghana, Mali, Burkina Faso, Malawi na Msumbiji ni baadhi ya nchi ambazo pia zimeingia katika mpango huo.

No comments

Theme images by Xaviarnau. Powered by Blogger.