BILL GATES ATOA US$350M KUSAIDIA SEKTA MBALIMBALI IKIWEMO KILIMO

Mfanyabiashara tajiri kutoka marekani Bill Gates ambae pia ni mwenyekiti wa Bill & Melinda Gates, amefanya mazungumzo rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. John Pombe Magufuli ikulu jijini Dar es salaam leo. Katika mazungumzo hayo;moja ya maafikiano yaliyofikiwa ni kutoa fedha kiasi cha Dola za marekani US$350 Milioni(Zaidi ya Bilioni 777) kwa ajili ya kuwezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo kilimo.




Katika sekta ya kilimo ambayo kiasi kikubwa cha fedha hizo kitatolewa kulenga miradi ya maendeleo ya kilimo; Bwana Gates ameeleza dhamira yake ya kutoa fedha hizo kupitia taasisi ya Bill and Melinda Gates foundation ni kusaidia uzalishaji wa mbegu bora za mazao ya kilimo na kuongeza uzalishaji mashambani. 


Nae Rais wa Tanzania, Mh John Pombe Magufuli amempongeza na kumshukuru Bwana Gates kuonyesha nia ya kusaidia Tanzania katika miradi ya maendeleo na kusisitiza fedha hizo zitasimamiwa vema kuhakikisha zinatumika sawa na malengo tajwa.

No comments

Theme images by Xaviarnau. Powered by Blogger.