WAKULIMA 30,000 UPATA MICHE YA CHIKICHI

Takribani wakulima 30,000 mkoani Kigoma watafaidika na hatua ya Taasisi kuinua na kusaidia sekta binafsi (PASS) kuanzisha hatua ya kuongeza uzalishaji wa mazao ya biashara kwa kipindi cha miaka mitatu(3). Manager wa PASS mkoa wa Kigoma bwana Faustine Mungo, akiongea na waandishi wa habari amesema wakulima hao watafaidika kwa kupata mbegu za zao la chikichi chini ya taasisi za kijamii ya Seed Change Tanzania(SCT) ambayo imepata fedha kutoka PASS.


Bwana Mungo amesema SCT imefanikiwa kuingiza miche ya mbegu za chikichi zaidi ya 60,000 kutoka Costa Rica ambayo itagawiwa kwa wakulima hadi mwisho wa mwaka huu. Amesisitiza kuwa lengo lilikua kuwafikia wakulima 10,000 kabla ya mwisho wa mwaka huu. PASS imefanikiwa kuwasaidia wakulima kupitia miradi mbalimbali yenye thamani ya Bilioni 13.2 katika kanda ya magharibi yenye inayohudumia mikoa (3) ambayo ni Tabora, Kigoma na Katavi.

No comments

Theme images by Xaviarnau. Powered by Blogger.