MBEGU MPYA YA ZAO LA ALIZETI YAZALISHWA
Mkuu wa mkoa wa Manyara Mh. Joel bendera amewaagiza wakulima mkoani humo kutumia mbegu mpya za alizeti zilizozalishwa hivi karibuni zenye ubora na
uzalishaji unaofikia gunia 18-25 kwa ekari zaidi ukilinganisha na mbegu za sasa
zinazozalisha kiasi cha magunia 5-7 kwa ekari.
Akiwasilisha agizo hilo kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa
Manyara; Mkuu wa wilaya ya Babati Mh. Raymond Mushi kwa wakulima na wadau wa
kilimo, wakati wa uzinduzi wa mpango wa kilimo biashara na mifumo ya masoko
kupitia mbegu mpya utakaotekelezwa ndani ya miaka 5. Mpango huo unaosimamiwa na
nchi 4 yaani Denmark, Sweden, Uswizi na Ireland utawahusisha wakulima katika
wilaya ya Babati, Hanan, Mbulu na Simanjiro.

No comments