WAFUGAJI SIMANJIRO WAANZISHA MASHAMBA YA NYASI
Wafugaji kutoka wilaya ya simanjiro wameanzisha mashamba ya
nyasi kwa ajili ya ulishaji wa mifugo na kuiomba serikali kuwapatia maeneo ya
ardhi ambayo hayaendelezwi kwa ajili ya kuendeleza uzalishaji wa nyasi. Wafugaji
wilayani humo wamesema hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la serikali
la kubadili mfumo wa ufugaji na kuboresha maeneo ya malisho ya mifugo ambao utasaidia
kupunguza na kuondoa migogoro baina ya wafugaji na wakulima.
Mbunge wa Simanjiro Mh. James Ole Milia amesema hatua hiyo
ni mwanzo mzuri na ukombozi kwa wafugaji na itawasaidia kuweka akiba ya malisho, kuongeza uzalishaji wa bidhaa za mifugo na kuongeza ubora wake pia, na kufuga kwa tija. Mkakati huo
ukifanikiwa utakua mfano wa kuigwa kwa wafugaji katika maeneo mengine nchini.

Enter your comment...bigup honorable milia,we support you all the way from Kenya
ReplyDelete